Dosari za Kifonolojia Zinazojitokeza kwa Wangoni Wanapojifunza Kiswahili
Keywords:
Dosari, kifonolojiia, Kiswahili, WangoniAbstract
Utafiti huu ulichunguza dosari za kifonolojia zinazojitokeza kwa
jamii ya Wangoni wanapojifunza Kiswahili. Tatizo la utafiti
lilichochewa na watafiti wengi kutafiti dosari kwa Wabantu
wanapojifunza lugha ya pili yenye mfumo tofauti na lugha yao ya
kwanza. Utafiti uliongozwa na Nadharia ya Uchanganuzi Dosari ya
Corder (1967)inayoeleza kwamba dosari katika ujifunzaji wa lugha
ya pili hazitokani tu na mifumo tofauti kati ya lugha ya kwanza na
lugha ya pili, bali kuna masuala anuwai mengine yanayomzunguka
mjifunzaji na kuchangia kuibuka kwa dosari. Utafiti ulikusanya
data katika wilaya ya Songea vijijini katika shule za sekondari
Nalima na Liganga. Utafiti ulihusisha jumla ya watoataarifa 24
ambao ni wanafunzi wanaosoma kidato cha tatu pamoja na walimu
wanaofundisha Kiswahili katika shule hizo. Mbinu zilizotumika
kukusanya data ni majadiliano ya kundi na hojaji. Uchambuzi wa
data za utafiti huu umetumia mbinu ya maelezo ambapo dosari zote
zilizobainika ziliwekwa katika makundi maalum na kutolewa
maelezo kikamilifu. Matokeo yanaonesha kwamba zipo dosari za
kifonolojia zinazojitokeza kwa Wangoni wanapojifunza Kiswahili,
hususani upachikaji wa sauti, mfano neno, afurika, sauti /u/
inapachikwa ubadilishaji wa sauti, mfano miladi badala ya
‘’miradi’’ na udondoshaji, mfano neno akuna badala ya ‘hakuna’.
Ili kuwafanya wajifunzaji hawa wajifunze Kiswahili kwa usahihi,
ilipendekezwa kuwa, kuwepo na mchanganyiko wa wanafunzi
kutoka ndani na nje ya mkoa katika shule za kata, kuwepo kwa
midahalo, makongamano na majarida ya Kiswahili ya kutosha, pia
yafanyike mazoezi shirikishi kwa shule zaidi ya moja
Downloads
Published
Issue
Section
License
Copyright (c) 2026 Africa Journal of Language Studies

This work is licensed under a Creative Commons Attribution-NonCommercial-NoDerivatives 4.0 International License.